• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Blogu |
    • Malalamiko |
Chemba District Council
Chemba District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Chemba

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Chemba DC Profile
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati
    • Hali Ya Uwekezaji
    • Kata, Vijiji na Vitongoji
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Divisheni
      • Elimu ya Awali na Msingi
        • Shughuli
        • Machapisho
      • Elimu ya Sekondari
        • Shughuli
        • Machapisho
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
        • Shughuli
        • Machapisho
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Mipango na Uratibu
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijiji na Mijini
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Takwimu
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Maliasili na Hifadhi ya Mazingira
      • Huduma za Sheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka, na Usafi wa Mazingira
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Mikopo 10%
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • Kudhibiti Maambukizi ya Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Siku za Kuonana na Mhe. Mwenyekiti
  • Miradi
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
    • Idhinishwa
  • Machapisho
    • Sheria
      • Permanent act
      • Ada na Ushuru
    • Ripoti
    • Fomu
      • Imprest
      • Masurufu
      • Hati miliki ya kiwanja
      • Likizo
      • Maombi ya leseni ya biashara
      • Fomu ya Kujiunga na Bima ya Afya
      • Ruhusa
    • Miongozo
      • Waraka wa mavazi kwa Watumishi wa Umma
      • Watumishi nje ya kituo
      • Kanuni za maadili za Madiwani
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

DARASA LA SABA CHEMBA WAAHIDI UFAULU KWA 100%

Posted on: September 5th, 2025

Wanafunzi wa darasa la saba Halmashauri ya Wilaya ya Chemba wameahidi  kufanya vizuri katika mtihani wao wa kuhitimu elimu ya msingi kwa asilimia  100%.


Ahadi hiyo imetolewa katika hafla ya  chakula cha pamoja iliyoambatana na maombi maalum pamoja na nasaha  kutoka kwa Mwakilishi wa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya, Ofisi ya Mkurugenzi,  Wazazi, Wazee maarufu, Viongozi wa Serikali ya Kijiji na Kata,  na Viongozi wa Dini.


 Hafla hiyo ya chakula cha pamoja imeongozwa na Mwakilishi wa Mkuu wa Wilaya ya Chemba Bi  Juster Katemana katika Shule ya Msingi Kidoka,  Shule ya Msingi Kwamtoro hafla hiyo imeongozwa na Katibu Tawala wa Wilaya Bi Salah Ngalingasi,  Shule ya Msingi Churuku hafla hiyo imeongozwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya  Chemba Ndugu Hassan Mnyikah, na Shule ya Msingi Goima ameongoza AfisaTarafa wa  Tarafa ya Goima Bi Joyce Olotu.


Akiongea katika Shule ya Msingi Kidoka  ambapo alikua Mgeni Rasmi akimwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Chemba  Bi Juster Katemana amesema    Halmashauri ya Wilaya ya Chemba ilitenga siku ya tarehe 4, Septemba 2025 kuwa ni siku ya Wazazi, Walimu,Wanafunzi, Kamati za Shule, Wazee maarufu , Viongozi wa Kata na Vijiji, na Viongozi wa Dini  kupata chakula cha pamoja  kuwaombea na kuwatia moyo Wanafunzi wa darasa la saba ambao  wanatarajia kufanya mtihani wa Taifa  tarehe 10 -11, Septemba 2025.


 Bi. Juster Katemana amewasihi Wanafunzi hao kujisomea kwa bidi katika siku hizi chache zilizobakia ambapo pia amewasisitiza  Wanafunzi hao kuendelea kumuomba Mungu kila mmoja kwa Imani yake ili waweze kufanya vizuri Zaidi.


Mwakilishi huyo wa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya amemshukuru Afisa Elimu Msingi Ndugu  Josephat Ambilikile  kwa maandalizi ya tukio hilo muhimu.


Aidha, Bi Juster Katemana amewashukuru Wazazi kwa ushirikiano waliounyesha pamoja na kuchangia chakula cha Wanafunzi hao ambacho kimewawezesha Wanafunzi hao kuendelea na masomo yao wakiwa na afya njema.


Mwakilishi huyo wa Mkuu wa Wilaya akatumia fursa hiyo kuwaomba Wazazi kutowakatisha Watoto tamaa pale watakapofaulu kwenda Sekondari na kuongeza kuwa Watoto wote watakaofaulu waende Shule hata kama watakua hawajapata sare za shule.


Akizungumza kwa niaba ya Wanfunzi wenzake Mwanafunzi Sabrati Abasi amewashukuru Wazazi, Walimu, Mwakilishi wa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya, Ofisi ya Mkurugenzi, Viongozi wa dini, Viongozi wa Serikali ya Kijiji na Kata kwa kujumuika nao  katika chakula cha pamoja, na  kuwaombea ili waweze kufanya vizuri katika mitihani yao.


 “Nakuhakikishia  Mwakilishi wa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya kuwa Wanafunzi wote wa darasa la saba katika shule ya msingi Kidoka tutafaulu kwa sababu Walimu wetu wametuandaa vizuri,  na tumefanya mitihani  ya kutosha “ amesema Sabrati Abasi.

Matangazo ya Kawaida

  • MAPOKEZI YA FEDHA July 22, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 22, 2025
  • KILA LA KHERI DARASA LA SABA 2025 September 09, 2025
  • WITO WA USAILI August 01, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • DC OKASH AONGOZA WAOMBOLEZAJI KUAGA MWILI WA BENJAMINI GEROME

    September 11, 2025
  • MNYIKAH AONGOZA TIMU YA WATAALAM KUKAGUA MIRADI CHEMBA

    September 08, 2025
  • DARASA LA SABA CHEMBA WAAHIDI UFAULU KWA 100%

    September 05, 2025
  • "TUMESHIRIKI, TUMESHINDA NA TUMEKABIDHI USHINDI"

    September 03, 2025
  • Angalia Zote

Video

Soya auction
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Forms
  • Frequently asked questions

Tovuti Muhimu

  • TCU
  • Tamisemi
  • National Examination Council
  • Government Website
  • Ministry of Finance
  • Mfumo wa Taarifa za Elimu

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji Tovuti

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Chemba District Council

    Sanduku la Posta: 830 CHEMBA

    Simu ya Mezani: 0262360175

    Simu ya Mkononi: 0765980765

    Barua pepe: ded@chembadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Chemba . Haki zote zimehifadhiwa.