• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Blogu |
    • Malalamiko |
Chemba District Council
Chemba District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Chemba

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Chemba DC Profile
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati
    • Hali Ya Uwekezaji
    • Kata, Vijiji na Vitongoji
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Divisheni
      • Elimu ya Awali na Msingi
        • Shughuli
        • Machapisho
      • Elimu ya Sekondari
        • Shughuli
        • Machapisho
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
        • Shughuli
        • Machapisho
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Mipango na Uratibu
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijiji na Mijini
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Takwimu
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Maliasili na Hifadhi ya Mazingira
      • Huduma za Sheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka, na Usafi wa Mazingira
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Mikopo 10%
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • Kudhibiti Maambukizi ya Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Siku za Kuonana na Mhe. Mwenyekiti
  • Miradi
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
    • Idhinishwa
  • Machapisho
    • Sheria
      • Permanent act
      • Ada na Ushuru
    • Ripoti
    • Fomu
      • Imprest
      • Masurufu
      • Hati miliki ya kiwanja
      • Likizo
      • Maombi ya leseni ya biashara
      • Fomu ya Kujiunga na Bima ya Afya
      • Ruhusa
    • Miongozo
      • Waraka wa mavazi kwa Watumishi wa Umma
      • Watumishi nje ya kituo
      • Kanuni za maadili za Madiwani
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

TIMU YA WATAALAMU WA HALMASHAURI YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO CHEMBA

Posted on: October 15th, 2025


Timu ya Wataalam wa Halmashauri ya Wilaya ya Chemba tarehe  15, Oktoba 2025 imefanya ukaguzi wa miradi  ya maendeleo sekta ya Afya na Elimu robo ya kwanza Julai – Septemba 2025/2026

Ujenzi wa wa Kituo shikizi cha thawekwa kilichopo Kijiji cha Porobanguma Kata ya Kwamtoro ni miongoni mwa miradi iliyokaguliwa  ambapo kituo hiki kinahusisha ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa  na Ofisi kwa jumla ya  fedha kiasi cha shlingi milioni  27,200,000, milioni 25,000,000 kutoka Serikali Kuu na milioni 2,200,000 kutoka mfuko wa Jimbo.

Kituo hiko   shikizi cha Thawekwa kwasasa  kimefikia hatua ya kuezekwa na kina jumla ya Wanafunzi 300 wa darasa la awali hadi darasa la tatu  na Walimu 3 tu.

kufuatia hali ya kusuasua kwa ujenzi wa kituo hiko kutokana na nguvu kazi hafifu kutoka kwa Wakazi wa eneo hilo  Timu ya Wataalam kutoka halmashauri imewataka viongozi wa  Kijiji cha Porobanguma kuendelea kuhamasisha Wakazi wa Kijiji hiko na kuhakikisha ujenzi wa kituo hiko unakamilika kabla ya msimu wa mvua kuanza.

Katika hatua nyingine Timu hiyo ya Wataalam imeitaka Kamati ya ujenzi wa Kituo cha Walimu (Teachers Resources Centre)kuwashirikisha Wananchi wa eneo hilo ili waweze kuchangia nguvu kazi pamoja  kufanya kazi kwa ukaribu na Kitengo cha manunuzi pamoja na maeneo mengine ndani ya Halmashauri ambayo yametekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo ili waweze kupata uzoefu na kushirikiana katika kutatua changamoto zinazowakwamisha  katika utekelezaji wa mradi huo.

Ujenzi wa kituo cha Walimu ambao upo katika hatua za walia za ujenzi  (Teachers Resources Centre)kinachojengwa Kata ya Farkwa  unahusisha ujenzi wa vyumba viwili na matundu mawili ya vyoo kwa fedha kiasi cha shilingi milioni 46,000,000 kutoka Serikali Kuu.

Aidha, Timu hiyo ya Wataalam imeipongeza  Serikali kwa  uboreshaji wa Jengo la Wazazi na watoto wachanga hususan Watoto wanaozaliwa kabla ya umri( Njiti) katika Hospitali ya Wilaya lililofanyiwa maboresho kwa fedha kiasi cha shilingi milioni 25,000,000 fedha kutoka Serikali Kuu  ili kuimarisha na kuboresha mazingira ya utoaji wa huduma  kwa Wazazi na Watoto wachanga.

Hata hivyo, Timu  hiyo ya Wataalam ilikamilisha ziara yake ya ukaguzi wa miradi katika ujenzi wa Shule mpya ya mkondo mmoja na nyumba ya Walimu 2 in 1 unaofanyika eneo la Chemba mjini kwa fedha kiasi cha shilingi milioni 397,200,000 (BOOST)

Ujenzi wa mradi huuu ambao uko katika hatua za awali unatarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwaka huu  ili shule hiyo ipokee wanafunzi wapya wa madarasa ya awali na msingi ikiwa ni pamoja na kupunguza mlundikano wa Wanafunzi katika shule ya msingi Chemba mwaka ujao 2026.

Matangazo ya Kawaida

  • MAPOKEZI YA FEDHA July 22, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 22, 2025
  • KILA LA KHERI DARASA LA SABA 2025 September 09, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI KWA WAOMBAJI WA KAZI YA UKUSANYAJI MAPATO October 03, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • TIMU YA WATAALAMU WA HALMASHAURI YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO CHEMBA

    October 15, 2025
  • “DHAMIRA YA SERIKALI NI KUPUNGUZA AU KUMALIZA KABISA VIFO VINAVYOTOKANA NA UZAZI”

    October 02, 2025
  • CRDB KANDA YA KATI YAKABIDHI MADAWATI 20 KWA SHULE YA MSINGI CHEMBA

    October 02, 2025
  • BONANZA LA MICHEZO CHEMBA DC VS KONDOA DC

    October 27, 2025
  • Angalia Zote

Video

Soya auction
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Forms
  • Frequently asked questions

Tovuti Muhimu

  • TCU
  • Tamisemi
  • National Examination Council
  • Government Website
  • Ministry of Finance
  • Mfumo wa Taarifa za Elimu

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji Tovuti

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Chemba District Council

    Sanduku la Posta: 830 CHEMBA

    Simu ya Mezani: 0262360175

    Simu ya Mkononi: 0765980765

    Barua pepe: ded@chembadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Chemba . Haki zote zimehifadhiwa.