• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Blogu |
    • Malalamiko |
Chemba District Council
Chemba District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Chemba

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Chemba DC Profile
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati
    • Hali Ya Uwekezaji
    • Kata, Vijiji na Vitongoji
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Divisheni
      • Elimu ya Awali na Msingi
        • Shughuli
        • Machapisho
      • Elimu ya Sekondari
        • Shughuli
        • Machapisho
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
        • Shughuli
        • Machapisho
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Mipango na Uratibu
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijiji na Mijini
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Takwimu
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Maliasili na Hifadhi ya Mazingira
      • Huduma za Sheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka, na Usafi wa Mazingira
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Mikopo 10%
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • Kudhibiti Maambukizi ya Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Siku za Kuonana na Mhe. Mwenyekiti
  • Miradi
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
    • Idhinishwa
  • Machapisho
    • Sheria
      • Permanent act
      • Ada na Ushuru
    • Ripoti
    • Fomu
      • Imprest
      • Masurufu
      • Hati miliki ya kiwanja
      • Likizo
      • Maombi ya leseni ya biashara
      • Fomu ya Kujiunga na Bima ya Afya
      • Ruhusa
    • Miongozo
      • Waraka wa mavazi kwa Watumishi wa Umma
      • Watumishi nje ya kituo
      • Kanuni za maadili za Madiwani
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Kikao maalum cha Halmashauri kuu ya CCM Wilaya ya Chemba chafanyika

Posted on: September 2nd, 2018

Na Shani Amanzi,

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Dodoma Ndg, Godwin Mkama amewataka Wanachama wa CCM waache tabia ya muingiliano wa kimaslahi badala yake wachape kazi kwani Chama cha Mapinduzi kipo kwa ajili ya kuendeleza shughuli za kimaendeleo na kudumisha amani ya Nchi.

Ndg, Godwin Mkama amesema Serikali ya Awamu ya Tano ya Mhe. Rais Dkt.John Pombe Magufuli inataka Wananchi wake wa ngazi zote wafaidike na huduma za kijamii zinazotolewa na Serikali, ndiyo maana kunakuwa na ubunifu wa kubana matumizi kwa mfano ujenzi wa vituo vya afya na shule kwa kutumia mafundi waliopo maeneo husika (Force Acount) bila kutumia wakandarasi na ni vema Waheshimiwa Madiwani mkasimamia ipasavyo fedha hizo.

Mkama aliyazungumza hayo kwenye Kikao Maalum cha Halmashauri Kuu ya CCM Wilaya ya Chemba na wanachama wa CCM, tarehe 1/9/2018 katika Ukumbi wa Godown ambapo alikuwa mgeni rasmi.

‘’Nawapongeza kwa kuanza kujenga ofisi ya chama, chama kuwa na ushirikiano mzuri baina ya Mhe. Mkuu wa Wilaya, Mhe. Mwenyeki wa Halmashauri, Mkurugenzi Mtendaji, Mhe. Mbunge, Wataalam, na mnafanya vizuri sana kuhakikisha mnatatua kero za Wananchi”aliongeza kwa kusema hivyo Ndg.Mkama.

Wakati huo huo Mhe. Mwenyekiti wa CCM mkoa aliwapokea wanachama wapya sita waliotoka vyama vya upinzani na kujiunga na Chama Cha Mapinduzi (CCM). Wanachama hao ni Abdallah Ally Suti (aliyekuwa Mwenyeki wa Chama cha CUF Wilaya ya Chemba), Msongoli Yahaya (aliyekuwa Mkurugenzi wa fedha wa Chama cha CUF Wilaya ya Chemba), Salim Juma Idonga ( aliyekuwa katibu kata wa Chama Cha Chadema kata ya Kidoka), Hussein Saidi Maimbi ( aliyekuwa katibu wa tawi wa Chama Cha CUF, tawi la kijiji cha Olboloti), Abasi Nkundulo (aliyekuwa katibu wa tawi wa Chama cha CUF, tawi la kijiji cha Mwaikisabe), William Suki (aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama cha CUF kijiji cha Muungano).

Aidha Mbunge wa Jimbo la Chemba Mhe.Juma Nkamia amesema Chemba ina tatizo kubwa la maji na amewaomba Wataalam wa Halmashauri wa Idara ya maji waendelee kupambana ili kuhakikisha wananchi wanapata maji maeneo yote na ameahidi kuchangia ujenzi wa Jengo la CCM Wilaya ya Chemba.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Chemba Mhe.Simon Odunga amesema Wilaya ya Chemba inatekeleza miradi mbalimbali ikiwemo ‘’kukarabati  majosho matatu katika vijiji vya Paranga, Rofati na Kidoka kwa Tshs. 1,316,000/=, pia msimu wa kilimo 2017/2018 uzalishaji wa chakula ulikuwa tani 106,652.4 na mazao ya kimkakati  katika kuongezea wananchi kipato  ni Alizeti, pamba na korosho.”

Mhe.Odunga amesema mafanikio hayo ya kiuchumi na kijamii inafanya Chama cha Mapinduzi kuendelea kuaminika kwa wananchi na CCM itaendelea kusimamia utekelezaji wa Miradi mbalimbali ya kiuchumi na kutoa huduma za kijamii kwa ukaribu zaidi.


Matangazo ya Kawaida

  • CHEMBA DC STRATEGIC PLAN July 01, 2024
  • Matokeo ya Sensa ngazi ya Kata Mwaka 2022 July 01, 2024
  • Chanjo-Halmashauri ya Wilaya ya Chemba June 01, 2024
  • Mapokezi ya fedha za Miradi Chemba DC June 27, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • ORODHA YA MAJIMBO MAPYA NA YALIYOBADILISHWA MAJINA

    May 12, 2025
  • RATIBA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI.

    May 08, 2025
  • Mwenyekiti Tume Huru ya Chaguzi (NEC) Aongoza kikao cha Kuthibitisha Mgawanyo Jimbo la Chemba Siku ya Tarehe April 27, 2025.

    April 28, 2025
  • Wasira aelezea faida za Muungano kwa wananchi wa Chemba

    April 27, 2025
  • Angalia Zote

Video

Soya auction
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Forms
  • Frequently asked questions

Tovuti Muhimu

  • TCU
  • Tamisemi
  • National Examination Council
  • Government Website
  • Ministry of Finance
  • Mfumo wa Taarifa za Elimu

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji Tovuti

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Chemba District Council

    Sanduku la Posta: 830 CHEMBA

    Simu ya Mezani: 0262360175

    Simu ya Mkononi: 0765980765

    Barua pepe: ded@chembadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Chemba . Haki zote zimehifadhiwa.