• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Blogu |
    • Malalamiko |
Chemba District Council
Chemba District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Chemba

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Chemba DC Profile
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati
    • Hali Ya Uwekezaji
    • Kata, Vijiji na Vitongoji
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Divisheni
      • Elimu ya Awali na Msingi
        • Shughuli
        • Machapisho
      • Elimu ya Sekondari
        • Shughuli
        • Machapisho
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
        • Shughuli
        • Machapisho
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Mipango na Uratibu
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijiji na Mijini
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Takwimu
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Maliasili na Hifadhi ya Mazingira
      • Huduma za Sheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka, na Usafi wa Mazingira
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Mikopo 10%
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • Kudhibiti Maambukizi ya Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Siku za Kuonana na Mhe. Mwenyekiti
  • Miradi
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
    • Idhinishwa
  • Machapisho
    • Sheria
      • Permanent act
      • Ada na Ushuru
    • Ripoti
    • Fomu
      • Imprest
      • Masurufu
      • Hati miliki ya kiwanja
      • Likizo
      • Maombi ya leseni ya biashara
      • Fomu ya Kujiunga na Bima ya Afya
      • Ruhusa
    • Miongozo
      • Waraka wa mavazi kwa Watumishi wa Umma
      • Watumishi nje ya kituo
      • Kanuni za maadili za Madiwani
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

KIKAO CHA WADAU WA ELIMU WILAYA YA CHEMBA TAREHE 05/01/2018.

Posted on: January 7th, 2018

KIKAO CHA WADAU WA ELIMU WILAYA YA CHEMBA CHAFANYIKA TAREHE  05/01/2018.

Na Shani Amanzi,

Mkuu wa Wilaya ya Chemba Mhe.Simon Odunga amewataka Watumishi wa Umma kutimiza wajibu wao maofisini na kuachana na kasumba ya kukimbia kazini kwa changamoto wanazozipata badala yake waboreshe mikakati waliyonayo ya kiutendaji ili kuweza kufikia tija ya kuwa na elimu bora  siyo bora elimu shuleni katika Wilaya ya Chemba.

Mhe.Odunga aliongeza “tuheshimu kazi zetu, nidhamu iwepo kwenye kazi, hatuwezi kuwa na Viongozi wa Idara halafu hatufanyi vizuri shuleni kama Serikali tunahakikisha tunalinda Usalama wa Watumishi wa Serikali na nyie Watumishi mnapaswa kuwa makini na jamii inayowazunguka na msijihusishe na mambo yasiyo ya msingi yakawachafua ’’

Aidha Mhe.Odunga amesema lazima mwaka huu waingie mkataba na Waratibu Elimu Kata  ambao kwa sasa ni (Maafisa Elimu Kata) ili waone tofauti kwenye matokeo ya darasa la saba mwaka 2018 na  utaratibu wa kuwapa chakula cha mchana shuleni wanafunzi unatakiwa kurudi katika Shule za Msingi na Sekondari.

Kwa upande wa Afisa Elimu Msingi Ndg.Modest Tarimo amesema pamoja na sababu nyingine, uhaba wa Walimu, upungufu wa madarasa, nyumba za Walimu na Matundu ya vyoo katika Shule za Msingi zimesababisha Wilaya ya Chemba kupata wastani wa asilimia 52  kwenye matokeo ya darasa la saba mwaka 2017 na kuwa ya mwisho kimkoa kati ya Wilaya 08.

“ Mwaka 2018 malengo ni kufaulisha kwa asilimia 80 katika ngazi ya Wilaya na asilimia 90 kwa upande wa Shule na kata ikiwa ni pamoja na kupunguza daraja D na E kwenye matokeo ya mitihani ya kitaifa”alisisitiza Ndg. Tarimo.

Naye Kaimu Afisa Elimu Sekondari Ndg. Hausi Mkwachu amesema kuna upungufu wa vitabu vya kiada na ziada hususani vya masomo ya sanaa na upungufu wa Walimu wa masomo ya Sayansi na Hisabati hivyo kusababisha Wilaya ya Chemba kupata wastani wa asilimia 54  katika matokeo ya kidato cha IV mwaka 2016 lakini kwa upande wa kidato cha VI mwaka  2017 wilaya ya Chemba ilipata asilimia 100 na kuwa ya kwanza kimkoa.

Pia Mbunge wa jimbo la Chemba Mhe. Juma Nkamia aliongeza kwa kusema “ili kuboresha ufaulu kwa Wanafunzi inatakiwa kutoa Elimu kwa Wananchi kabla hatujawaomba michango kwa ajili ya maendeleo  shuleni kwasababu kuna  dhana waliyonayo kuwa Elimu ni bure”.

Hata hivyo Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Chemba Dkt.Semastatus amesema “Kamati za shule, bodi za shule, Vikao vya WDC, na Mikutano ya kijiji iwe na agenda ya Elimu katika vikao vyao ili kuzungumzia changamoto za Elimu katika shule zao na kuzitatua”.

Dkt.Mashimba amesema kumekuwepo na Wadau wengi wa Elimu lakini Wafanyakazi wa Elimu wasitumie vigezo vya fedha za miradi kuwepo au kutokuwepo ndiyo sababu ya kukwama maendeleo ya shule za msingi na sekondari wilayani bali wanapaswa kufanya kazi kwa kuzingatia sheria, taratibu na miongozo iliyopo.

Kikao cha Wadau wa Elimu kimehusisha Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya ya Chemba ambaye ni Mwenyekiti wa  Kikao hicho, Katibu Tawala, Mheshimiwa Mwenyekiti wa Halmashauri ya Chemba, Mheshimiwa Mbunge wa jimbo la Chemba, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Chemba, waheshimiwa Madiwani wa Chemba, Wathibiti ubora wa Shule, Chama cha Walimu, Waratibu Elimu, Wakuu wa Shule, Walimu Wakuu na Wakuu wa Idara kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Chemba .

Matangazo ya Kawaida

  • CHEMBA DC STRATEGIC PLAN July 01, 2024
  • Matokeo ya Sensa ngazi ya Kata Mwaka 2022 July 01, 2024
  • Chanjo-Halmashauri ya Wilaya ya Chemba June 01, 2024
  • Mapokezi ya fedha za Miradi Chemba DC June 27, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • ORODHA YA MAJIMBO MAPYA NA YALIYOBADILISHWA MAJINA

    May 12, 2025
  • RATIBA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI.

    May 08, 2025
  • Mwenyekiti Tume Huru ya Chaguzi (NEC) Aongoza kikao cha Kuthibitisha Mgawanyo Jimbo la Chemba Siku ya Tarehe April 27, 2025.

    April 28, 2025
  • Wasira aelezea faida za Muungano kwa wananchi wa Chemba

    April 27, 2025
  • Angalia Zote

Video

Soya auction
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Forms
  • Frequently asked questions

Tovuti Muhimu

  • TCU
  • Tamisemi
  • National Examination Council
  • Government Website
  • Ministry of Finance
  • Mfumo wa Taarifa za Elimu

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji Tovuti

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Chemba District Council

    Sanduku la Posta: 830 CHEMBA

    Simu ya Mezani: 0262360175

    Simu ya Mkononi: 0765980765

    Barua pepe: ded@chembadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Chemba . Haki zote zimehifadhiwa.