• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Blogu |
    • Malalamiko |
Chemba District Council
Chemba District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Chemba

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Chemba DC Profile
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati
    • Hali Ya Uwekezaji
    • Kata, Vijiji na Vitongoji
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Divisheni
      • Elimu ya Awali na Msingi
        • Shughuli
        • Machapisho
      • Elimu ya Sekondari
        • Shughuli
        • Machapisho
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
        • Shughuli
        • Machapisho
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Mipango na Uratibu
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijiji na Mijini
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Takwimu
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Maliasili na Hifadhi ya Mazingira
      • Huduma za Sheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka, na Usafi wa Mazingira
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Mikopo 10%
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • Kudhibiti Maambukizi ya Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Siku za Kuonana na Mhe. Mwenyekiti
  • Miradi
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
    • Idhinishwa
  • Machapisho
    • Sheria
      • Permanent act
      • Ada na Ushuru
    • Ripoti
    • Fomu
      • Imprest
      • Masurufu
      • Hati miliki ya kiwanja
      • Likizo
      • Maombi ya leseni ya biashara
      • Fomu ya Kujiunga na Bima ya Afya
      • Ruhusa
    • Miongozo
      • Waraka wa mavazi kwa Watumishi wa Umma
      • Watumishi nje ya kituo
      • Kanuni za maadili za Madiwani
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

JAMII YAHIMIZWA KUSHIRIKIANA KATIKA UNYONYESHAJI NA MALEZI YA WATOTO

Posted on: August 7th, 2025

"Maziwa ya mama pekee kwa miezi sita ya mwanzo yana umuhimu wake katika jamii, yanamjenga mtoto kiakili na kimwili,  na humuepusha mtoto na hali ya udumavu, Mtoto akiwa  mdumavu hali ya utendaji wake  na kufikiria inakua hairidhishi"


Hayo yamebainishwa na Mganga Mkuu wa Wilaya ya Chemba Dkt.Marko Mgonja  wakati akizingumza na akinamama waliohudhuria kilele cha maadhimisho ya  wiki ya unyonyeshaji yaliyofanyika katika kituo cha huduma ya Mama na Mtoto kilichopo kijiji cha Mirambo Kata ya Goima Wilaya ya Chemba.


"Afya ya mama na mtoto ni muhimu sana, Sisi Sekta ya afya huwa tunatoa maelekezo kwamba mama anapojihisi ana ujauzito anatakiwa chini ya miezi mitatu yeye na mwenza wake ahudhurie kiliniki ili apate mafunzo juu ya namna bora ya kulea mimba ili mtoto atakayezaliwa awe na afya bora na baada ya kujifungua mama anaelekezwa namna ya kumnyonyesha mtoto wake" amesema Dkt. Mgonja


Aidha, Mganga Mkuu huyo amezungumzia suala uzazi wa mpango na kuwasihi akina mama kuwa ili mtoto aweze kunyonya vizuri anahitaji muda wa kuwa karibu na mama yake hivyo amewasihi akina mama kuzingatia  njia za uzazi wa mpango ili mtoto apate haki yake ya msingi ya kunyonya vizuri na kukua vizuri.


"Mama anayenyonyesha au mwenye ujauzito anahitaji faraja, anahitaji kupumzika na  apunguziwe kazi, hivyo hili ni suala La jamii nzima tushirikiane kwa pamoja kuhakikisha mama anayenyonyesha anapata muda wa kutosha wa kumnyonyesha mtoto" Amesema Dkt. Mgonja.


Dkt.Mgonja pia amewahamasisha kina mama wa Mirambo kujiunga katika vikundi na  kuchangamkia fursa ya  mikopo ya 10% ya Vijana, Wanawake na Watu wenye ulemavu inayotolewa na  Halmashauri ili waweze kufanya shughuli mbalimbali zitakazowaingizia kipato na kujiimarisha kiuchumi.


Hata hivyo Dkt. Mgonja amewasihi kina mama kuepuka kujifungulia nyumbani, au kwa Wakunga wa Jadi na badala yake watumie Vituo vya huduma za afya kwa usalama zaidi wa mama na Mtoto na kuongeza kuwa Serikali inaendelea kuboresha vituo vya huduma za afya ili kuhakikisha Jamii inakua salama kwa kupata huduma bora za afya.


Akihitimisha maadhimisho ya wiki ya unyonyeshaji Afisa lishe wa Wilaya Bi  Faith Temu ameshukuru shirika La Compassion pamoja na Viongozi wa dini Kijiji cha Mirambo kwa kuunga mkono Juhudi za Serikali ili kuimarisha huduma ya mama na mtoto na kuwaomba kina mama wote waliohudhuria kilele cha wiki ya unyonyeshaji kuwa mabalozi kwa kina  mama wengine katika maeneo yao kuhusu umuhimu wa unyonyeshaji ili  Wilaya ya Chemba iweze kuwa na kizazi chenye afya bora.


Thamini Unyonyeshaji; weka mazingira wezeshi kwa Mama na Mtoto


#Lishe ya mwanao, mafanikio yake#  Kujaza tumbo si lishe, jali unachomlisha.








Matangazo ya Kawaida

  • MAPOKEZI YA FEDHA July 22, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 22, 2025
  • WITO WA USAILI August 01, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • JAMII YAHIMIZWA KUSHIRIKIANA KATIKA UNYONYESHAJI NA MALEZI YA WATOTO

    August 07, 2025
  • KUELEKEA UCHAGUZI MKUU 2025 WASIMAMIZI WASAIDIZI NGAZI YA KATA WATAKIWA KUZINGATIA MATUMIZI YA VIFAA, UBANDIKAJI WA MABANGO NA ORODHA YA WAPIGA KURA

    August 06, 2025
  • WASIMAMIZI WASAIDIZI WA UCHAGUZI NGAZI YA KATA JIMBO LA CHEMBA WAPATIWA MAFUNZO

    August 04, 2025
  • WAHAMASISHENI WAZAZI/WALEZI WACHANGIE CHAKULA SHULENI

    July 30, 2025
  • Angalia Zote

Video

Soya auction
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Forms
  • Frequently asked questions

Tovuti Muhimu

  • TCU
  • Tamisemi
  • National Examination Council
  • Government Website
  • Ministry of Finance
  • Mfumo wa Taarifa za Elimu

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji Tovuti

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Chemba District Council

    Sanduku la Posta: 830 CHEMBA

    Simu ya Mezani: 0262360175

    Simu ya Mkononi: 0765980765

    Barua pepe: ded@chembadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Chemba . Haki zote zimehifadhiwa.