• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Blogu |
    • Malalamiko |
Chemba District Council
Chemba District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Chemba

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Chemba DC Profile
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati
    • Hali Ya Uwekezaji
    • Kata, Vijiji na Vitongoji
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Divisheni
      • Elimu ya Awali na Msingi
        • Shughuli
        • Machapisho
      • Elimu ya Sekondari
        • Shughuli
        • Machapisho
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
        • Shughuli
        • Machapisho
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Mipango na Uratibu
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijiji na Mijini
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Takwimu
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Maliasili na Hifadhi ya Mazingira
      • Huduma za Sheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka, na Usafi wa Mazingira
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Mikopo 10%
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • Kudhibiti Maambukizi ya Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Siku za Kuonana na Mhe. Mwenyekiti
  • Miradi
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
    • Idhinishwa
  • Machapisho
    • Sheria
      • Permanent act
      • Ada na Ushuru
    • Ripoti
    • Fomu
      • Imprest
      • Masurufu
      • Hati miliki ya kiwanja
      • Likizo
      • Maombi ya leseni ya biashara
      • Fomu ya Kujiunga na Bima ya Afya
      • Ruhusa
    • Miongozo
      • Waraka wa mavazi kwa Watumishi wa Umma
      • Watumishi nje ya kituo
      • Kanuni za maadili za Madiwani
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

DED CHEMBA AWAPONGEZA WALIMU KWA MATOKEO MAZURI YA KUDATO CHA SITA 2025

Posted on: July 16th, 2025

Mkurugenzi Mtendajiwa Halmashauri ya Wilaya ya Chemba Ndugu Hassan Mnyika  ametoa pongezi hizo  katika hafla fupi ya kuwapongeza Walimu wa shule zilizofanya vizuri katika mtihani wa kidato cha sita 2025 iliyofanyika Julai 16, 2025 katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri.


"Kwa dhati ya moyo wangu leo nimefurahi sana, nawapongeza sana,ninawashukuru sana, mmenivika nguo na mmeniheshimisha,ninawaahidi kushirikiana  nanyi bega kwa bega  ili tuweze kufanya vizuri zaidi" amesema Mkurugenzi Mnyika.


Ndugu Mnyika amewaomba Walimu hao pamoja na mazingira magumu waliyonayo wasikate tamaa, waendelee kujitumi na mafanikio haya waliyoyapata wayashikilie na walenge kupata  ufaulu wa juu zaidi, wafanye kila linalowezekana  ambapo pia amewaahidi ushirikiano na kuwatembelea katika maeneo yao mara kwa mara ili waweze kujadili kwa pamoja mambo  muhimu yahusuyo sekta hiyo muhimu ya elimu.


Mapema akizungumza katika hafla hiyo Mkuu wa divisheni ya elimu ya Sekondari Bi. Jeanimina Mtitu amesema kuwa ufaulu wa juu ndio mpango mzima  hivyo amewataka Walimu hao  wajikite katika kuangalia ubora wa ufaulu ambapo ameongeza kuwa matamanio yake mwakani 2026 ni kuifanya Chemba ichukue nafasi tatu za mwanzo Kimkoa.


"Ndugu zangu tumekutana hapa Leo kwa jambo Moja tu kufurahi, kula na kunywa, mwakani tunaweza kwenda mbali zaidi hata Zanzibar kupongezana kama tutafanya vizuri zaidi" amesema Bi Jeanimina


Kwa upande wake Afisa taaluma Sekondari Bi Bernadetha Akaro amesema kuwa ufaulu kwa Shule  unaonesha kuwa Shule ya Sekondari Msakwalo inaongoza  kwa kuwa na wastani wa alama za gredi (GPA) ya 1.8669 ikifuatiwa na Shule ya Sekondari Soya  ikiwa na GPA  ya 2.3759 na Shule ya Sekondari ya Mondo imeshika nafasi tatu ikiwa na GPA ya 2.7469 Kiwilaya.


Sambamba na hilo Mtaaluma huyo amesema kuwa  katika matokeo hayo ya kidato cha sita 2025 jumla ya Wanafunzi 307 wamepata daraja La kwanza, 114 daraja la pili, Wanafunzi 40 wamepata daraja La tatu na Mwanafunzi 1 amepata daraja la 4.


Aidha, Bi  Bernadetha amebainisha kuwa Shule ya Sekondari  Msakwalo kwa mwakani 2024 ilipata ufaulu  wa GPA ya 2.0527 wakati mwaka 2025 ubora wa ufaulu ni 1.8669, Shule hii Kimkoa imeshika nafasi ya 3 wakati mwaka 2024 ilishika pia nafasi ya 3 ambapo Kitaifa imeshika nafasi ya 62.


Bi Bernadetha amesema kuwa kiujumla Halmashauri ya Wilaya ya Chemba imekua ya kwanza Kimkoa kwa miaka miwili mfululizo, mwaka 2024 ubora wa ufaulu ulikua ni 2.3393 na mwaka 2025 ubora wa ufaulu ni 2.3299.


Akihitimisha taarifa ya tathimini ya matokeo ya kidato cha sita 2025 Mtaaluma Huyo ameeleza kuwa mafanikio hayo mazuri yametokana na jitihada za Walimu ambapo wametoa ushirikiano na kujituma katika kutekeleza mikakati yote iliyowekwa ili kufanikisha lengo la Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe. Rais  Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuboresha viwango vya ufaulu katika sekta hiyo muhimu ya Elimu.


Matangazo ya Kawaida

  • CHEMBA DC STRATEGIC PLAN July 01, 2024
  • Matokeo ya Sensa ngazi ya Kata Mwaka 2022 July 01, 2024
  • Chanjo-Halmashauri ya Wilaya ya Chemba June 01, 2024
  • Mapokezi ya fedha za Miradi Chemba DC June 27, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • DED CHEMBA AWAPONGEZA WALIMU KWA MATOKEO MAZURI YA KUDATO CHA SITA 2025

    July 16, 2025
  • "DC CHEMBA AWATAKA WATENDAJI KUITISHA MIKUTANO YA WANANCHI"

    July 15, 2025
  • DC CHEMBA ASIKILIZA NA KUJIBU KERO ZA WANANCHI KATA YA CHANDAMA NA SONGOLO

    July 10, 2025
  • "NENDENI MKAFANYE KAZI KWA BIDII, MZINGATIE TARATIBU ZA UTUMISHI WA UMMA, NA MBORESHE VIWANGO VYA UFAULU"

    July 09, 2025
  • Angalia Zote

Video

Soya auction
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Forms
  • Frequently asked questions

Tovuti Muhimu

  • TCU
  • Tamisemi
  • National Examination Council
  • Government Website
  • Ministry of Finance
  • Mfumo wa Taarifa za Elimu

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji Tovuti

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Chemba District Council

    Sanduku la Posta: 830 CHEMBA

    Simu ya Mezani: 0262360175

    Simu ya Mkononi: 0765980765

    Barua pepe: ded@chembadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Chemba . Haki zote zimehifadhiwa.