• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Blogu |
    • Malalamiko |
Chemba District Council
Chemba District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Chemba

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Chemba DC Profile
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati
    • Hali Ya Uwekezaji
    • Kata, Vijiji na Vitongoji
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Divisheni
      • Elimu ya Awali na Msingi
        • Shughuli
        • Machapisho
      • Elimu ya Sekondari
        • Shughuli
        • Machapisho
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
        • Shughuli
        • Machapisho
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Mipango na Uratibu
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijiji na Mijini
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Takwimu
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Maliasili na Hifadhi ya Mazingira
      • Huduma za Sheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka, na Usafi wa Mazingira
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Mikopo 10%
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • Kudhibiti Maambukizi ya Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Siku za Kuonana na Mhe. Mwenyekiti
  • Miradi
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
    • Idhinishwa
  • Machapisho
    • Sheria
      • Permanent act
      • Ada na Ushuru
    • Ripoti
    • Fomu
      • Imprest
      • Masurufu
      • Hati miliki ya kiwanja
      • Likizo
      • Maombi ya leseni ya biashara
      • Fomu ya Kujiunga na Bima ya Afya
      • Ruhusa
    • Miongozo
      • Waraka wa mavazi kwa Watumishi wa Umma
      • Watumishi nje ya kituo
      • Kanuni za maadili za Madiwani
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

"DC CHEMBA AWATAKA WATENDAJI KUITISHA MIKUTANO YA WANANCHI"

Posted on: July 15th, 2025

Mkuu wa Wilaya ya Chemba Mhe. Halima Okash amewataka Watendaji wa Vijiji na Kata kuitisha mkutano na  kuwasomea Wananchi  mapato na matumizi  pamoja na kuwafahamisha kuhusu fedha zilizopokelewa na miradi itakayotekelezwa kutokana na fedha hizo.


DC Okash ameyasema hayo Julai 15, 2025 akiwa katika ziara ya kusikiliza na kutatua kero za Wananchi Kata ya Makorongo na Kata ya Gwandi Wilayani Chemba.


"Wananchi wana haki ya kujua fedha zinazopokelewa, miradi  iliokusudiwa na kufuatilia ubora wa miradi hiyo kama inaakisi gharama halisi " Amesema DC Okash.


Aidha Mhe. Okash amesema Serikali ya awamu ya sita  inayoongozwa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imewekeza fedha nyingi katika sekta ya elimu ili kuwawezesha Watoto wote kupata elimu bure kuanzia ngazi ya msingi, na sekondari ambapo pia Serikali inatoa mikopo kwa elimu ya juu, hivyo amewataka Wazazi na Walezi  kuzitafuta fursa za elimu kwa Watoto kwakuwa urithi mzuri wa Mtoto ni elimu  ili aweze kujisimamia na kuwasaidia Wazazi kusimamia shughuli za maendeleo.


"Chemba itajengwa na Wanachemba wenyewe, Chemba haitajengwa na Wageni somesheni Watoto wenu waje kuwasaidia kusimamia maendeleo katika Wilaya yenu" Amesema Mhe. Okash.


Sambamba na hilo, Mkuu huyo wa Wilaya  amesema kuwa Serikali ngazi ya Wilaya inatarajia kufanya sensa ya  mifugo na utambuzi wa Wakulima ambapo pia amewataka  Wafugaji kufuga kisasa na Wakulima kulima  kisasa na kuachana na ufufugaji na kilimo cha mazoea  


Hata hivyo, Mtendaji wa Kata ya Makorongo Ndugu  Andrew Chilewa amemshukuru Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hssan kwa kuwezesha utekelezaji wa miradi mbalimbali katika Kata hiyo  ikiwa ni pamoja na miradi ya Afya, miradi ya elimu, Maji, barabara   na kupeleka Watumishi 12 ambao wanaendelea kuwatumikia Wananchi.



Matangazo ya Kawaida

  • CHEMBA DC STRATEGIC PLAN July 01, 2024
  • Matokeo ya Sensa ngazi ya Kata Mwaka 2022 July 01, 2024
  • Chanjo-Halmashauri ya Wilaya ya Chemba June 01, 2024
  • Mapokezi ya fedha za Miradi Chemba DC June 27, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • DED CHEMBA AWAPONGEZA WALIMU KWA MATOKEO MAZURI YA KUDATO CHA SITA 2025

    July 16, 2025
  • "DC CHEMBA AWATAKA WATENDAJI KUITISHA MIKUTANO YA WANANCHI"

    July 15, 2025
  • DC CHEMBA ASIKILIZA NA KUJIBU KERO ZA WANANCHI KATA YA CHANDAMA NA SONGOLO

    July 10, 2025
  • "NENDENI MKAFANYE KAZI KWA BIDII, MZINGATIE TARATIBU ZA UTUMISHI WA UMMA, NA MBORESHE VIWANGO VYA UFAULU"

    July 09, 2025
  • Angalia Zote

Video

Soya auction
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Forms
  • Frequently asked questions

Tovuti Muhimu

  • TCU
  • Tamisemi
  • National Examination Council
  • Government Website
  • Ministry of Finance
  • Mfumo wa Taarifa za Elimu

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji Tovuti

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Chemba District Council

    Sanduku la Posta: 830 CHEMBA

    Simu ya Mezani: 0262360175

    Simu ya Mkononi: 0765980765

    Barua pepe: ded@chembadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Chemba . Haki zote zimehifadhiwa.