• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Blogu |
    • Malalamiko |
Chemba District Council
Chemba District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Chemba

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Chemba DC Profile
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati
    • Hali Ya Uwekezaji
    • Kata, Vijiji na Vitongoji
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Divisheni
      • Elimu ya Awali na Msingi
        • Shughuli
        • Machapisho
      • Elimu ya Sekondari
        • Shughuli
        • Machapisho
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
        • Shughuli
        • Machapisho
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Mipango na Uratibu
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijiji na Mijini
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Takwimu
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Maliasili na Hifadhi ya Mazingira
      • Huduma za Sheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka, na Usafi wa Mazingira
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Mikopo 10%
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • Kudhibiti Maambukizi ya Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Siku za Kuonana na Mhe. Mwenyekiti
  • Miradi
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
    • Idhinishwa
  • Machapisho
    • Sheria
      • Permanent act
      • Ada na Ushuru
    • Ripoti
    • Fomu
      • Imprest
      • Masurufu
      • Hati miliki ya kiwanja
      • Likizo
      • Maombi ya leseni ya biashara
      • Fomu ya Kujiunga na Bima ya Afya
      • Ruhusa
    • Miongozo
      • Waraka wa mavazi kwa Watumishi wa Umma
      • Watumishi nje ya kituo
      • Kanuni za maadili za Madiwani
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

DC CHEMBA ASIKILIZA NA KUJIBU KERO ZA WANANCHI KATA YA CHANDAMA NA SONGOLO

Posted on: July 10th, 2025

DC CHEMBA ASIKILIZA NA KUJIBU KERO ZA WANANCHI KATA YA CHANDAMA NA  SONGOLO.


Mkuu wa Wilaya ya Chemba Mhe. Halima Okash Julai 10, 2025 amefanya ziara ya kusikiliza na kujibu kero za Wananchi wa Kata ya Chandama na Kata ya Songolo Wilayani Chemba.


Mara baada ya kujibu kero za Wakazi wa Kata hizo DC  Halma Okash amewataka Wakazi wa Kata hizo kubadili mtazamo wao kuhusu elimu,waone umuhimu wa elimu kwa Watoto wao ili kuwatengenezea mazingira mazuri ya kujitegemea na kuongeza kuwa hakuna urithi mzuri kwa Watoto zaidi ya elimu.


Sambamba na hilo DC Okash amewasisitiza Wazazi kuhusu umuhimu wa kuchangia chakula cha Watoto wao Shuleni ili kuongeza kiwango cha uelewa na ufaulu kwani ni vigumu sana kwa Watoto kusoma na kuelewa vizuri masomo yao wakiwa na njaa.


DC Okash pia amewaomba Wazazi kuwapa ushirikiano Walimu ili waweze kuwasomesha vizuri Watoto  badala ya kuwavunja moyo Walimu hao.


Kuhusu utunzaji na ufuatiliji wa miradi ya maendeleo Mhe. Okash amesema kuwa Wananchi wanao wajibu wa kutunza  na kufuatilia utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika maeneo yao kwani Serikali inatumia fedha  nyingi katika utekelezaji wa miradi hiyo ili iweze kutumika kwa muda mrefu.


Aidha, Mhe. Okash amekemea  vitendo vya ukatili wa kijinsia, ubakaji, unyanyasaji na vitendo vyote vinavyoenda kinyume na maadili.


Vilevile Mkuu huyo wa Wilaya ya Chemba ametoa onyo kwa Wafugaji wanaolisha mifugo yao kwenye mashamba ya Wakulima na kusema kuwa Serikali ngazi ya Wilaya imejipanga kikamilifu kuwashughulikia Wafugaji wote wataokaoenda kinyume na agizo la Serikali.


Akizungumzia kuhusu suala la Maronjoo, DC Okash amesema kuwa Serikali ngazi ya Wilaya tayari imeanza oparesheni ya kuwakamata Maronjoo hivyo amewataka Wazazi kuzungumza na na Watoto wao wenye tabia hizo kuacha mara moja.


Akihitimisha ziara yake DC Okash amesema kuwa Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imefanya mambo makubwa katika Wilaya ya Chemba ikiwa ni pamoja na utekelezaji wa miradi ya maendeleo  kama vile miradi ya elimu. Afya, maji, umeme, barabara, ruzuku kwa Walengwa wa TASAF na mikopo ya 10% kwa Vijana, Wanawake na Watu wenye ulemavu hivyo amewaomba Wakazi wa Kata ya Chandama na Kata ya Songolo kujitokeza kwa wingi na kupiga kura katika uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika mwezi Oktoba, 2025.

Matangazo ya Kawaida

  • CHEMBA DC STRATEGIC PLAN July 01, 2024
  • Matokeo ya Sensa ngazi ya Kata Mwaka 2022 July 01, 2024
  • Chanjo-Halmashauri ya Wilaya ya Chemba June 01, 2024
  • Mapokezi ya fedha za Miradi Chemba DC June 27, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • DC CHEMBA ASIKILIZA NA KUJIBU KERO ZA WANANCHI KATA YA CHANDAMA NA SONGOLO

    July 10, 2025
  • "NENDENI MKAFANYE KAZI KWA BIDII, MZINGATIE TARATIBU ZA UTUMISHI WA UMMA, NA MBORESHE VIWANGO VYA UFAULU"

    July 09, 2025
  • TANGAZO NAFASI ZA KUSIMAMIA UCHAGUZI MKUU 2025.

    July 01, 2025
  • MATOKEA MCHUJO RMA

    June 22, 2025
  • Angalia Zote

Video

Soya auction
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Forms
  • Frequently asked questions

Tovuti Muhimu

  • TCU
  • Tamisemi
  • National Examination Council
  • Government Website
  • Ministry of Finance
  • Mfumo wa Taarifa za Elimu

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji Tovuti

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Chemba District Council

    Sanduku la Posta: 830 CHEMBA

    Simu ya Mezani: 0262360175

    Simu ya Mkononi: 0765980765

    Barua pepe: ded@chembadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Chemba . Haki zote zimehifadhiwa.