• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Blogu |
    • Malalamiko |
Chemba District Council
Chemba District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Chemba

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Chemba DC Profile
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati
    • Hali Ya Uwekezaji
    • Kata, Vijiji na Vitongoji
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Divisheni
      • Elimu ya Awali na Msingi
        • Shughuli
        • Machapisho
      • Elimu ya Sekondari
        • Shughuli
        • Machapisho
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
        • Shughuli
        • Machapisho
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Mipango na Uratibu
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijiji na Mijini
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Takwimu
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Maliasili na Hifadhi ya Mazingira
      • Huduma za Sheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka, na Usafi wa Mazingira
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Mikopo 10%
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • Kudhibiti Maambukizi ya Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Siku za Kuonana na Mhe. Mwenyekiti
  • Miradi
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
    • Idhinishwa
  • Machapisho
    • Sheria
      • Permanent act
      • Ada na Ushuru
    • Ripoti
    • Fomu
      • Imprest
      • Masurufu
      • Hati miliki ya kiwanja
      • Likizo
      • Maombi ya leseni ya biashara
      • Fomu ya Kujiunga na Bima ya Afya
      • Ruhusa
    • Miongozo
      • Waraka wa mavazi kwa Watumishi wa Umma
      • Watumishi nje ya kituo
      • Kanuni za maadili za Madiwani
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

ATHARI ZA MAFURIKO WILAYANI CHEMBA.

Posted on: January 15th, 2018

Na Shani Amanzi,

Mkuu wa Wilaya ya Chemba Mhe.Simon Odunga ametoa agizo kwa Wananchi wa Wilaya ya Chemba katika kata ya Mrijo wanaoishi mabondeni kuhama maeneo hayo kama alivyoagiza Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe.Binilith Mahenge alipotembelea kata hiyo tarehe 9/1/2018.

Mhe. Odunga alisema hayo alipofanya ziara ya kuangalia hali inavyoendelea katika kata ya Mrijo tarehe 10/1/2018 alipokuwa na Kamati ya Maafa ya Wilaya ya Chemba.

Wilaya ya Chemba imeanza kupata mvua za msimu kuanzia mwezi Novemba 20 katika maeneo machache na mvua hizi zimekuwa za wastani na juu ya wastani ambapo mpaka sasa ni mm 232 na hivyo kusababisha madhara kwa baadhi ya Wananchi na mali zao.

Kata ya Mrijo ni miongoni mwa maeneo yaliyopata madhara makubwa ya mvua zilizonyesha kuanzia usiku wa tarehe 8-9/1/2018 katika vijiji vya Kaloleni ,Mrijo chini na Olboloti .

Maeneo mengine yaliyopata madhara ni kata ya Chemba katika kijiji cha Chambalo ambapo nyumba 60 zilizingirwa na maji na ng’ombe 14 walizama katika kijiji cha Mondo kata ya Mondo kutokana na mvua zilizonyesha.

Miundombinu ya barabara za Chemba-Kiteto ,Chandama-Soya ,Kimaha-Soya zimeharibika na hazipitiki kabisa wakati barabara za Kwamtoro –Sanzawa ,Kwamtoro-Lahoda,Cheku-Kelema zimeharibika na hazipitiki kwa urahisi.Pia huduma ya umeme na maji safi na salama katika vijiji vya Kaloleni ,Mrijo chini na Olboloti hazipatikani.

Madhara haya yamesababisha kifo cha kijana mmoja mwenye umri wa miaka 35 aitwaye Teo Sekali wa kijiji cha Mwaikisabe kata ya Kimaha.

Kwa ujumla taarifa hii ni ya awali ikielekeza hali halisi ilivyokuwa katika eneo la tukio mpaka sasa,athari zilizojitokeza ,changamoto,hatua zilizochukuliwa ,idadi kamili ya wahanga na mahitaji yao.

KIJIJI
IDADI YA NYUMBA ZILIZOANGUKA KUTOKANA NA MAJI
IDADI YA NYUMBA ZILIZOZINGIRWA NA MAJI
KAYA ZILIZOATHIRIKA
IDADI YA WATU WALIOATHIRIKA
MAHITAJI YA CHAKULA KWA WAATHIRIKA KWA SIKU 30(TANI)
MALI ZILIZOHARIBIKA
OLBOLOTI
87
650
270
1698
-Tani 30 za nafaka,Tani 15 za mazao jamii ya mikunde, Lita 1000 ,sukari kg 530, Chumvi 6oo
-Mahindi gunia 25na debe3,Alzeti gunia 1 na debe3,kuku 26,Bata 7,Mbuzi 7,Ng’ombe 2 na maharage debe 3
KALOLENI
26
27
28
196
-Tani 4 za nafaka,tani 2 za mimea jamii ya mikunde,lita 100 za
Mafuta ya kupikia ,sukari kg 20,chumvi kg 50
-Tani 4 za Nafaka,tani 2 za mimea jamii ya mikunde,lita 100 za mafuta ya kupikia,sukari kg 20,chumvi kg 50
JUMLA
122
679
307
1943
-TANI 35 ZA MAHINDI

Hatua za awali zilizochukuliwa na timu ya Maafa ya Wilaya na kata ni kuwahamisha watu wote wenye nyumba zilizozingirwa na maji, wananchi waliokosa makazi walihifadhiwa kwa ndugu/jamaa na wengine walihifadhiwa katika madarasa ya shule ya msingi Mrijo chini. Pia mali za waathirika wa mafuriko ziliorodheshwa na kuhifadhiwa kwenye maghala ya Olboloti na Mrijo chini kwa usalama zaidi.

Vilevile, Jeshi la zima moto na uokoaji Mkoa wa Dodoma lilifanikiwa kutoa huduma ya uokoaji wa kaya 31 katika kitongoji cha Kaloleni walioshindwa kuvuka maji. Wahanga waliandikishwa majina na Wenyeviti wa Vitongoji chini ya utaratibu wa kamati ya maafa ya wilaya na masomo kwenye shule ya Sekondari Mrijo na kituo cha utayari Kaloleni yalisitishwa mpaka hapo hali itapokuwa shwari.

Changamoto walizokumbana nazo Kamati ya maafa kuanzia mwanzo wa tukio ni uhaba wa vyombo vya usafiri mfano magari, baadhi ya Wananchi kutotii maagizo toka kwa Viongozi ya kuwataka kuhama maeneo hatarishi,Wilaya kukosa vyombo vya uokoaji kwa ajili ya kutoa huduma kwa wakati na hivyo kusubiri vifaa kutoka Mkoani, kuharibika kwa miundo mbinu ya barabara na kusababisha kuchelewesha utoaji wa huduma kwa wakati.

Mhe.Simon Odunga amezitaja hatua zilizochukuliwa na Uongozi wa Wilaya ya Chemba ni kutoa “gunia 20 za Unga wa mahindi,maharage gunia 5,sukari kg 100,mafuta ya kula lita100, vifaa tiba na water guard kwa ajili ya maji ya kunywa”

Aidha Mhe.Odinga amesema pamoja na hatua za awali zilizochukuliwa na Wilaya ,Kamati ya Maafa ya Wilaya inaomba kusaidiwa kupata mahitaji yalioanishwa kama ifuatavyo tani 35 za nafaka,tani 17.25 za mazao jamii ya mikunde,lita 113 za mafuta ya kula ,sukari kg 620,tanki 4 za lita 10000 za kuhifadhia maji,katoni 700 za maji ya kunywa,magodoro 1000,blanketi 1000 na dawa za vifaa tiba.

“ Wilaya ya Chemba inaendelea kufanya tathmini ya maeneo watakayohamishwa kwa ajili ya makazi waathirika wote wa mafuriko pamoja na kuwapatia huduma muhimu kama vile vyakula na ulinzi na tunapenda kutoa shukrani zetu za dhati kwa Mkuu wa Mkoa Mhe,Binilith Mahenge,Kamati yake ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa pamoja na Mbunge wa Jimbo la Chemba Mhe.Juma Nkamia kwa kufika katika kata ya Mrijo kuwafariji waathirika wa mafuriko”alihitimisha kwa kusema hayo Mhe.Simon Odunga.

Matangazo ya Kawaida

  • CHEMBA DC STRATEGIC PLAN July 01, 2024
  • Matokeo ya Sensa ngazi ya Kata Mwaka 2022 July 01, 2024
  • Chanjo-Halmashauri ya Wilaya ya Chemba June 01, 2024
  • Mapokezi ya fedha za Miradi Chemba DC June 27, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • ORODHA YA MAJIMBO MAPYA NA YALIYOBADILISHWA MAJINA

    May 12, 2025
  • RATIBA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI.

    May 08, 2025
  • Mwenyekiti Tume Huru ya Chaguzi (NEC) Aongoza kikao cha Kuthibitisha Mgawanyo Jimbo la Chemba Siku ya Tarehe April 27, 2025.

    April 28, 2025
  • Wasira aelezea faida za Muungano kwa wananchi wa Chemba

    April 27, 2025
  • Angalia Zote

Video

Soya auction
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Forms
  • Frequently asked questions

Tovuti Muhimu

  • TCU
  • Tamisemi
  • National Examination Council
  • Government Website
  • Ministry of Finance
  • Mfumo wa Taarifa za Elimu

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji Tovuti

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Chemba District Council

    Sanduku la Posta: 830 CHEMBA

    Simu ya Mezani: 0262360175

    Simu ya Mkononi: 0765980765

    Barua pepe: ded@chembadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Chemba . Haki zote zimehifadhiwa.