- Mwanzo
- Kuhusu Sisi
- Utawala
- Fursa za Uwekezaji
- Huduma Zetu
- Madiwani
- Miradi
- Machapisho
- Kituo cha Habari
Tarehe 05/ 12/2025 kupitia mkutano wa kwanza wa Baraza la Madiwani waliochaguliwa katika uchaguzi uliofanyika Oktoba, 2025 waliapishwa rasmi zoezi lililoenda sambamba na uchaguzi wa Mwenyekiti wa Halmashauri na Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Chemba.
Katika Uchaguzi huo Mhe Leba Raphael Paul Diwani wa Kata ya Ovada kupitia CCM amechaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Chemba kwa kupata kura 34 kati ya kura 36 zilizopigwa huku Mhe Halidi Ramadhani Iddi Diwani wa Kata ya Kimaha kupitia CCM amechaguliwa kuwa Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Chemba kwa kupata kura 35 kati ya kura 36 zilizopigwa.
Zoezi hilo lilisimamiwa na Bi Sara Ngalingasi Katibu Tawala wa Wilaya ya Chemba ambapo amewataka Madiwani hao kuzingatia nidhamu, uwazi, uwajibikaji, na kushirikiana kwa karibu na Wananchi wanaowatumikia.
Kuapishwa kwa Wahe. Madiwani pamoja na kumchagua Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri pamoja na kuundwa Kamati za kudumu za Halmashauri ni hatua inayoashiria kuanza rasmi utekelezaji wa majukumu ya Baraza katika Halmashauri katika kuwatumikia Wananchi wa Chemba
Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Chemba linaundwa na Madiwani 36, ambapo Madiwani 9 ni wa viti malum 26 ni wa Kata pamoja na Mbunge wa Jimbo la Chemba.
Chemba District Council
Sanduku la Posta: 830 CHEMBA
Simu ya Mezani: 0262360175
Simu ya Mkononi: 0765980765
Barua pepe: ded@chembadc.go.tz
Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Chemba . Haki zote zimehifadhiwa.