- Mwanzo
- Kuhusu Sisi
- Utawala
- Fursa za Uwekezaji
- Huduma Zetu
- Madiwani
- Miradi
- Machapisho
- Kituo cha Habari
“ATAKAYECHEZEA MAPATO YA HALMASHAURI, HUYO NI HALALI YANGU”
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri wa Wilaya ya Chemba Ndugu Hassan Mnyikah ametoa rai kuwa yeyote atakayecheza na mapato ya Halmashauri hawezi kumwachia kirahisi kwasababu uti wa mgongo wa Halmashauri ni ukusanyaji wa mapato.
Mnyikah ameyasema hayo Novemba 12, 2025 wakati wa kikao chake na Watendaji wote wa Kata na Vijiji wa Halmashauri ya Wilaya ya Chemba kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri.
“Tukikosa mapato Halmashauri haitaweza kufanya ktu,hivyo yeyote atakayecheza na mapato huyo siwezi kumwambia kwa ligha rahisi” amesema Mnyikah
Aidha, Mkurugenzi Mnyikah amewataka Watendaji Kata na Vijiji wa Halmashauri ya Wilaya ya Chemba kufuata sharia, taratibu, kanuni na miongozo ya matumizi ya fedha za Serikali ili kuiweka Halamashauri katika hali ya usalama.
Mnyikah pia amesisitiza suala la usimamizi wa miradi ya maendeleo katika Vijiji na Kata zote za Chemba na kuwataka Watendaji hao kuhakikisha wanafuata taratibu zote muhimu zinazotakiwa ili kuhakikisha miradi hiyo inatekelezwa kwa wakati sahihi na ubora unaotakiwa.
Akizungumzia ukusanyaji na usimamizi wa mapato kwa kipindi cha robo ya kwanza Julai – Septemba 2025/26 Mweka hazina (W) James Dalasia amesema Halmashauri ilitakiwa kukusanya kwa 25% lakini kutokana na juhudi za Watendaji hao Halmashauri imekusanya mapato kwa 30% na hivyo kuwa Halmashauri ya kwanza katika Mkoa wa Dodoma.
“Ninawapongeza sana Watendaji wote kwa namna mnavyopambana kuhakikisha Halmashauri inafikia malengo yake katika ukusanyaji wa mapato, nawaomba tuendelee na ushirikiano huo ili tuweze kufanya vizuri Zaidi kwa siku zijazo” amesema Mweka hazina (W) James Dalasia.
Mapema akimkaribisha Mkurugenzi Mnyikah kuzungumza na Watendaji hao Mkuu wa Idara ya Utumishi Ndugu Henry Mniachi amesema lengo la kikao hiko ni Mkurugenzi kufahamiana na Watendaji wote na pia kutoa maelekezo mahususi yatakayowawezesha Watendaji hao kutekeleza majukumu yao usahihi.
Hata hivyo, kufuatia kikao hiko Watendaji walimshukuru Mkurugenzi kwa kuitisha kikao hiko ambapo pia walipata fursa ya kuzungumzia changamoto mbalimbali zinazowakabili katika utekelezaji wa majukumu yao ikiwa ni pamoja na madai ya stahiki zao za msingi.
Chemba District Council
Sanduku la Posta: 830 CHEMBA
Simu ya Mezani: 0262360175
Simu ya Mkononi: 0765980765
Barua pepe: ded@chembadc.go.tz
Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Chemba . Haki zote zimehifadhiwa.